Kamisheni ya Utumishi wa Umma - ZanzibarKamisheni ya Utumishi wa Umma - ZanzibarKamisheni ya Utumishi wa Umma - Zanzibar
+255 (24) 2230034
kamisheni.utumishi@zpsc.go.tz
Zanzibar, Tanzania
Kamisheni ya Utumishi wa Umma - ZanzibarKamisheni ya Utumishi wa Umma - ZanzibarKamisheni ya Utumishi wa Umma - Zanzibar

KUWAAGA WASTAAFU

Ghafla ya Kuwaaga Wastaafu wa Kamisheni ya utumishi wa Umma

Katibu wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma ndugu Kabingwa Mashaka Simba amesema wataendeleza mambo mema na tabia njema wakiwa kazini na mahali  popote kwa kushirikiana pamoja na watendaji  wa Taasisi za serikali ili mafanikio yaweze kupatikana kwa kasi kubwa

Katibu Kabigwa ameyasema hayo katika hafla fupi  ya kuwaaga watumishi watatu waliostaafu  katika Kamisheni ya Utumishi wa Umma mwanakwerekwe

Amesema lengo la kuwafanyia sherehe  hiyo ni kuwakumbuka na kuthamini mchango wao walioutoa wakati walipokuwa kazini na kuishi nao vizuri katika muda wote utendaji wao.

Hata hivyo Katibu Kubingwa amesema wataendelea kuwatumia pale ambapo watahitaji  kupata ushauri  na mchango wao. Amesema kuondoka kwao ni jambo la lazima kwa kila mtumishi wa umma pale muda unapoisha wa kuitumikia Serikali.

Nae Mkurugenzi wa Utawala  RasilimaliWatu na Mipango bi  Maryam Rished  Mbarouk amesema  wastaafu hao  walikua wakitenda haki  katika utendaji wa majukumu yao  na kuwasaidia wafanyakazi wengine kwa kuwapa ushauri mzuri.

Aidha bi   Mryam amewapongeza kwa kuutumia muda wao vizuri hadi kufikia kustaafu kwa salama na amani ni jambo la kujivunia na kumshukuru Mungu kwani wengine hufanya  makosa hadi kufikia kufukuzwa kazi.

Wakitoa shukurani wastaafu hao wamewasisitiza watendendaji wezao kushirikiana pamoja katika kazi, kupendana  na kufuata sheri zote za kazi zilizowekwa  ikiwa kuwa na heshima na nidhamu pamoja na kutumia lugha nzuri.

Katika sherehe hiyo wastaafu hao   walikabidhiwa zawadi mbali mbali ikiwemo cheti cha nidhamu , TV flat, Feni, jagi la umeme, na mswala. Wastaafu wenyewe ni ndugu Ramadhan Mohammed Khamis, Hassan Ameir Hafidhi na  bi Fatma Mkubwa Makame.

Leave A Comment

Subscribe to our newsletter

Sign up to receive latest news, updates, promotions, and special offers delivered directly to your inbox.
No, thanks